wavuti.com Updates

-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

Napenda kuwataarifu kuwa blogu hii inapumzishwa rasmi na tovuti mpya imezaliwa kwa jina www.wavuti.com

This is to inform you that this blog has been retired. A new website to take her place is up and running at www.wavuti.com

Saturday, May 30, 2009

TweetThis! Qauli ya Umoja wa Wazalendo Kukhusu Kuzama Meli Malindi

Wazee wetu, Ndugu zetu,
Assalaam Alaaykum,

UMOJA, UHURU, UADILIFU
Qauli ya Umoja wa Wazalendo Kukhusu Msiba wa Kuzama Meli hapo Bandarini Malindi, Zanzibar; taarikhi 29.05.09.

Umoja wa Wazalendo, una wingi wa huzni kwa msiba uliotokea usiku wa jana, taarikhi 29 May, 2009; kwa kuzama meli hapo bandarini Malindi na kusababisha vifo, kupotea mali na kusababisha mashaka kwa abiria na kila aliekuwepo wakati huo. Haya ni maqadiri ya Mwenyezi Mungu Mtukufu Subhaanahu wa Taáala, linaloandikwa halizuiliki kutokea; bali lina sababu.

Hapana shaka huu ni msiba wetu sote, msiba wa kila Mzanzibari, ni msiba wa kila Muumini na kila binaadamu.

Tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu Subhaanahu wa Taáala awaghufirie makosa yao marehemu wetu, awalaze mahali pema, awatie Peponi kwa Rehma Zake, wao na jamii ya Waumini; na awazidishie subira na mapenzi wafiwa wote, Aamyn.

Huu ndio mwisho wetu sote, tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu Subhaanahu wa Taáala atujaalie mwisho mwema, sisi na jamii ya Waumini; Aamyn.

Mkono wetu wa taáazia tunaupeleka kwa Rais wa Zanzibar, Mhishimiwa Rais Aman Abeid Aman, Sirikali ya Zanzibar na wananchi wa Zanzibar kwa jumla.

إنّا لله و إنّا إليه راجعون

Mwenyezi Mungu Mtukufu Subhaanahu wa Taáala awajaalie marehemu wetu hawa ni miongoni mwa Mashahidi, Aamyn.

Wa Billahi Tawfiiq
Umoja wa Wazalendo
Zanzibar
May 30, 2009

0 feedback :

Recent Comments . Kauli za Wasomaji

###recentComment###

More Opportunities ads