wavuti.com Updates

-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

Napenda kuwataarifu kuwa blogu hii inapumzishwa rasmi na tovuti mpya imezaliwa kwa jina www.wavuti.com

This is to inform you that this blog has been retired. A new website to take her place is up and running at www.wavuti.com

Tuesday, January 06, 2009

TweetThis! Bibi Sarah Obama kuhudhuria maapisho ya mjukuu Barack Obama

Sarah Obama ambaye ni bibi yake raisi mtarajiwa wa Marekani, Barack Obama anatarajiwa kuwa mmoja wa mamilioni ya mashuhuda watakaoshiriki kwenye sherehe za kuapishwa kwa raisi wa Marekani hapo Januari 21.

Bibi Obama atakuwa mmoja wa wageni wa heshima na ataongozana na ujumbe maalum kutoka katika serikali ya Kenya, Umoja wa Afrika na wanadiplomasia wengine watakaopewa fursa ya kushiriki tafrija maalumu siku moja kabla ya tarehe ya kuapishwa Barack Obama kama raisi wa 44 wa Marekani. Waziri wa mambo ya nje wa Kenya pamoja na kikundi cha kwaya cha 'Boys Choir of Kenya' nao watasafiri kujumuika katika mwaliko huo utakaofanyika katika hoteli iliyopo mjini Washington.

Historia fupi ya Barack Obama inasema kuwa,  Barack alizaliwa katika jimbo la Hawaii kwa Mama mzungu Mmarekani na Baba Mwafrika MKenya aliyekuwa masomoni nchini Marekani. Baada ya masomo, Baba yake Barack aliondoka Marekani na kurejea nchini Kenya huku akimwacha Barack akiwa katika umri mdogo. Hadi Baba yake Barack anafariki mwaka 1982, Barack hakuwa akiwafahamu kwa karibu ndugu na jamaa zake mpaka alipofunga safari ya kuwatembelea huko Kenya mnano mwaka 2006.

Kwenye kitabu chache cha "Dreams from My Father", Barack anaeleza kuwa alikutana na kusabahiana na bibi yake (Sarah) kwa mara ya kwanza mwaka 1988. Ingawaje ilikuwa ni vigumu kuelewana lugha, bado waliweza kufahamiana katika mambo kadhaa. Obama katika kitabu chake hicho anaandika,
Our mutual vocabulary exhausted, we stared ruefully down at the dirt until (half-sister) Auma finally returned".
...and Granny then turned to Auma and said, in a tone I could understand, that it pained her not to be able to speak to the son of her son.
Bibi Obama anaishi katika kijiji cha Kogelo kilichoko Magharibi mwa Kenya na huzungumza lugha ya Luo na KiSwahili.

Kabla ya safari hii, Sarah Obama amewahi kuitembelea nchi ya Marekani mara mbili.

Ninamtakia safari njema yenye furaha za shamra shamra na sherehe za kuapishwa mjukuu wake kwa hatua na mafanikio aliyoyafikia hadi sasa (na pengine baadaye).

0 feedback :

Recent Comments . Kauli za Wasomaji

###recentComment###

More Opportunities ads