wavuti.com Updates

-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

Napenda kuwataarifu kuwa blogu hii inapumzishwa rasmi na tovuti mpya imezaliwa kwa jina www.wavuti.com

This is to inform you that this blog has been retired. A new website to take her place is up and running at www.wavuti.com

Monday, May 11, 2009

TweetThis! Iko siku kitaeleweka tu! Gold dust from Tanzania lands in India's customs net.

Kiiiiiila mwezi huwa inapigwa kelele katika vyombo vya habari na mawasiliano kuwa, "jama eh, mwatuibia na mnajua kuwa mnatuibia dhahabu yetu kwa kiini macho cha kupima udongo huko Bara Asia". Lengo lenu la kuiba mali asili zetu litaisha tarehe gani? Mnatudanganya na tumeshakuambieni kuwa tupo wachache tunaona na tunakerwa na udanganyifu wenu! Tukianza kuwafahamisha Wananchi kupitia vyombo vya habari mtadai tunaichafua Serikali na Uongozi wake na kwamba tunachochea vurugu isiyo na sababu. Tena huwa hamna dogo mnasema, 'leteni vithibitisho na nyaraka katika mamlaka husika kuhusu tuhuma hizo'. Mnajua fika kuwa si lolote si chochote bali kupotezeana muda na kukatishana tamaa tu. Hamna hata lepe la aibu viumbe ninyi. Mliumbwa umbwaje ninyi mnaoopigiwa kelele hizi muache kutuibia? ninyi ambao mliwaendea wananchi na kuwahadaa huku mkitumia lugha ya kuomba ridhaa yao muwaongoze (kumbe mna nia ya kuwatawala) sasa mnaziba masikio yenu kwa nta msisikie malalamiko yao? Mnachopenda ninyi ni kusifiwa sifa za uongo tu, viumbe msio na soni. Hadi habari zianze kuandikwa katika vyombo vya KiMataifa ndipo mseme mnaunda tume ya uchunguzi kisha muanze kurushiana mipira isiyokuwa na refarii?
Mlilogwa na nani ninyi lakini? Mmeingiliwa na pepo gani na mnapungwa vipi hayo mapepo?
Mungu wangu na Baba yangu, ni kwa nini hili li nchi lina viongozi wenye dharau, jeuri na ukatili wa hali ya juu hivi? Ni kiburi gani walizaliwa nacho hawa watu? Wametoka ukoo gani wa nchi yetu hasa ili wafae kutangazwa 'wa kuogopwa kama ugonjwa usiotibika'?
Lakini, iko siku kitaeleweka tu, nasema!
Gold dust from Tanzania lands in customs net 
Customs sleuths on Monday seized 2.786 kg of gold at Bengaluru International Airport (BIA); the gold was smuggled from Tanzania.

Singh from Ahmendabad and Mohammed Alla Baksh from Bangalore, who arrived from Dubai in an Emirates flight, have been arrested.

According to sources, Baksh ran a gold-polishing business in Bangalore. The gold brought by the duo was in `dust' form. After treating under heat, they would get over 85% pure gold.

The two left India for Africa on April 16. Although they claimed the gold was purchased from a mine in Ghana, the bills are from Tanzania. They did not have relevant documents for bringing the gold dust to India.

This was the third trip the two had made to African countries. They claimed their earlier visits were for `negotiations' and this was the first time they had brought gold. Later, they said they carried cash to Tanzania through which they purchased gold.

Carrying the gold dust, they went to Dubai on May 5 and stayed there for four to five days before finally flying to Bangalore.

Customs sleuths suspect a cartel of goldsmiths may be behind the purchase of gold dust. "They may have pooled in money and sent the two for purchasing the item," a customs official said. "We're investigating how they carried large amount of cash from India," the official added - TimesOfIndia.IndiaTimes.com/Bangalore

0 feedback :

Recent Comments . Kauli za Wasomaji

###recentComment###

More Opportunities ads