wavuti.com Updates

-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

Napenda kuwataarifu kuwa blogu hii inapumzishwa rasmi na tovuti mpya imezaliwa kwa jina www.wavuti.com

This is to inform you that this blog has been retired. A new website to take her place is up and running at www.wavuti.com

Monday, February 16, 2009

TweetThis! Cheka : Mwandishi amhoji Mfugaji

Mkulima amejiwa na mwaandishi wa magazeti kumuhoji kuhusu maisha ya shambani, na mkulima huyu hawapendi waandishi wa habari akaona bora amchoshe katika kujibu maswali, na mambo yakawa hivi:

MWANDISHI: Wewe unawalisha ng'ombe chakula gani?
MKULIMA: Ng'ombe yupi Mweupe au Mwekundu?
MWANDISHI: Ng'ombe mweupe
MKULIMA: Ninamlisha nyasi na viguta vya mahindi
MWANDISHI: Na mwekundu?
MKULIMA: Vile vile nyasi na viguta vya mahindi
MWANDISHI: ahaa sawa, na sehemu ya kulala ni wapi?
MKULIMA: Ng'ombe yupi mweupe au mwekundu?
MWANDISHI: Mweupeee!!!!
MKULIMA: Mweupe ninamlaza bomani kulee
MWANDISHI: Na mwekundu?
MKULIMA: Vile vile namlaza na mwenziwe.
MWANDISHI: Hii sehemu yote majumba mengi wakati wa kulisha unafanyaje?
MKULIMA: Yupi mweupe au mwekundu?
MWANDISHI: Woooteeee!!!! {kwa hasira}
MKULIMA: Mweupe ninamfunga kamba na kumzungusha malishoni na kumrudisha
MWANDISHI: Na mwekundu vilevile?
MKULIMA: Mwekundu? Mwekundu yeye ninamfunga kamba na kuzunguka nae kama mwenziwe tu.
MWANDISHI: Kwanini kila mara nikikuuliza huduma za ng'ombe wako unaniuliza mweupe au mwekundu halafu inatokea kuwa kazi zao wote ni sawa?????
MKULIMA: Kwa sababu ng'ombe mweupe ni wangu.
MWANDISHI: Na mwekundu?
MKULIMA: Na mwekundu ni wangu vilevile.

0 feedback :

Recent Comments . Kauli za Wasomaji

###recentComment###

More Opportunities ads