wavuti.com Updates

-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

Napenda kuwataarifu kuwa blogu hii inapumzishwa rasmi na tovuti mpya imezaliwa kwa jina www.wavuti.com

This is to inform you that this blog has been retired. A new website to take her place is up and running at www.wavuti.com

Sunday, December 14, 2008

TweetThis! Bush arushiwa kiatu cha hasira

Mwandishi wa habari, Muntadar al-Zeidi, raia wa Iraki ameshindwa kuvumilia na kujikuta akivua viatu vyake viwili na kuvirusha kimoja baada ya kingine kwa madhumuni ya kumlenga Raisi wa Marekani ndugu G.W. Bush katika mkutano aliokuwa nao na waansishi hao akiwa pamoja na mwenyeji wake Mhe. Waziri Mkuu wa Iraki, bw. Nuur al Maliki.
Inasemekana kuwa hasira za mwandishi wa habari zilitokana na kuuawa kwa rafiki, ndugu na jirani zake na yeye mwenyewe kusumbuliwa na askari wa Marekani katika mojawapo ya shughuli zake za uandishi. Mwandishi huyo alitamka maneno haya kabla ya kurusha viatu hivyo: "This is a goodbye kiss, you dog"
AP video link
Kwa mujibu wa wanahabari, katika mila ya KiArabu ni dharau ya hali ya juu kwa mtu kukuonesha soli ya kiatu wachilia mbali kukurushia kiatu chenyewe. Hii ndiyo sababu hasa ya baadhi ya watu kuvua ndala zao na kuikanyaga sanamu ya Saddam Hussein ilipoangushwa.
Mwandishi wa habari huyo na wengine wawili walikamatwa na wana usalama.

Baadhi ya maoni ya watu yanaonesha kukisifu kitendo hicho na kukiita cha kishujaa il hali baadhi ya watu wameshangazwa na kusema hii inaonesha ni kwa kiasi gani upo uzembe katika safu ya ulinzi nchini Iraki.

0 feedback :

Recent Comments . Kauli za Wasomaji

###recentComment###

More Opportunities ads